Share news tips with us here at Hivisasa

Mbunge wa Borabu, Ben Momanyi amesema mabadiliko na uteuzi wa mawaziri wapya katika serikali kuu uliofanywa na Rais Uhuru Kenyatta uliegemea kabila mbili na kubagua kabila zingine.

Kulingana na Momanyi, kila kabila inafaa kukumbukwa wakati serikali inateua viongozi au mawaziri katika nyadhifa kuu za serikali.

Akizungumza na mwandishi huyu siku ya Jumatano, Momanyi alisema uteuzi wa mawaziri uliofanywa siku ya Jumanne na Rais Uhuru Kenyatta hukuwa wa kufaa kwa kile alichokitaja kama ubaguzi wa kabila zingine.

"Kabila zote zinastahili kukumbukwa katika uteuzi wa nyandifa kuu za serikali lakini uteuzi wa rais ulionekana kuegemea kabila mbili,” alisema Momanyi.

Wakati huo huo, Momanyi ameiomba serikali kujaribu kila iwezalo kudhibiti ufisadi serikalini.

Rais Kenyatta alifanya mabadiliko katika nyadhifa za mawaziri na kuteua mawaziri wapya katika serikali yake, huku wizara moja ikiongezwa.

Baadhi ya wakazi katika Kaunti ya Nyamira walipongeza rais kwa uteuzi na mabadiliko aliofanya huku wakimwombwa kupambana na kero la ufisadi.

“Tunampongeza rais kwa kufanya mabadiliko katika wizara nchini. Sasa tunamwomba apambane na ufisadi ili Kenya iendelee mbele,” alisema Peterson Nyache, mkazi.