Do you have a lead on a newsworthy story? Share news tips with us here at Hivisasa!

Serikali ya jimbo la Nakuru imetumia zaidi ya shilingi milioni nane kufadhili vituo vitano vya matibabu katika jimbo ndogo la Njoro.

Akiongea Jumatano katika hafla ya kukabidhi wanafunzi sare za shule kwenye shule ya msingi ya Kapkembu kaunti ndogo ya Njoro, gavana Mbugua alisema kuwa kituo cha matibabu cha Kaptich kilipokea shilingi milioni mbili, huku maeneo ya Mauche, Taita, Teret na Kapkembu yakipata shilingi milioni 1.5 kila moja.

Alisema serikali ya jimbo lake inaangazia afya ya wakaazi katika jimbo hilo.

“Katika kipindi cha wiki moja ijayo serikali yangu itatoa dawa na vifaa vingine vya afya vinavyogharimu shilingi millioni 71,” Mbugua alisema.

Mwaka jana serikali ya jimbo la Nakuru ilisema ilitumia shilingi milioni 52 katika kufadhili ununuzi wa dawa na baadhi ya vifaa kwenye hospitali za kaunti.