Wakazi wa eneo bunge la Changamwe katika mtaa dumi wa Dunga Unuse wameshtumu mamlaka ya idara ya polisi pamoja na vijana ambao walihusika katika ubomoaji wa nyumba zao siku ya Jumanne asubuhi, ambapo zaidi ya familia 1,500 ziliachwa bila makao.

Is there a story unfolding in your community? Let Hivisasa know

Ubomoaji huo ulifanywa siku ya Jumanne mapema, ambapo vijana ambao inasemekana walikuwa pamoja na mafisa wa polisi waliweza kufanya shughuli hiyo kwa usimamizi wa mafisa hao wa polisi.

Kulingana na msemaji wa waathiriwa hao Samson Mutuku, eneo ambalo nyumba hizo zimejengwa bado limekuwa na mzozo kati ya wakazi na mwekezaji bunafsi ambaye amekuwa akitishia kuwa atabomoa makazi yaliyojengwa katika eneo hilo na kudai kuwa alinunua sehemu hiyo, hivyo basi wenyeji hao wamekaa katika eneo hilo kinyume cha sheria.

“Hii si haki hata kidogo kubomolewa makazi yetu kwani sisi si wakenya, tunataka serikali ya kaunti yetu ya Mombasa kuingilia suala hili na kutafuta suluhu,” alisema Mutuku.

Alisema kuwa si haki hata kidogo kamwe kwani eneo hilo linaaminika kuwa la umma, na kumshtumu mwekezaji huyo kwa kufanya ulaghai kwa kushirikiana na baadhi ya viongozi wa kisiasa kutoka eneo hilo ili kunyakua sehemu hiyo ambayo alisema wamekaa kwa muda mrefu.

Hata hivyo, waziri wa nyumba na ardhi katika kaunti ya Mombasa, akiongea na wandishi wa habari, aliwahakikishia wakazi hao kuwa suala hilo litashughulikiwa kwa dharura, na kuwataka wakazi kuwa na subira huku uchunguzi kuhusiana na kisa hicho ukifanywa.