Wazazi wa shule ya msingi ya Matutu wadi ya Gesima eneo bunge la Kitutu Masaba, wamempongeza mwanasiasa Mokaya Maroko kwa kuipatia shule hiyo gunia za mahindi.

Do you have a lead on a newsworthy story? Share news tips with us here at Hivisasa!

Wakiongea katika shule hiyo hapo jana wakati wa kupokezwa zawadi hiyo wazazi hao walimpomngeza mwanasiasa  huyo na kusema hiyo ni njia moja ya kuinua  viwango vya  masoma katika wadi ya Gesima .

“Tuko na shukrani kwa mheshimiwa Mokaya Maroko kwa kukumbuka shule yetu ya Matutu kwa kutupatia msaada wa mahindi ili wanafunzi wapate  chakula na kuendelea na masomo yao,” alisema  Salome Kenyoni mkaazi.

Aidha, wazazi hao wamewaomba viongozi wengine kuiga mfano huo na kufadhili miradi mbalimbali  ili kuinua viwango vya mandeleo hasa katika sekta ya elimu.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo  Patrick Nyangeri alipongeza hatua hiyo  iliyochukuliwa na Mokaya Maroko na kusema kuwa mahindi hayo  yatasaidia pakubwa katika muhula wa pili kwa kuwa wanafunzi watakuwa na chakula  cha kutosha ikilinganishwa na nyakati zilizopita.

Nyangeri, alisema kuwa  wakati wanafunzi huendea katika chakula cha mchana,  wengi wao hurudi shuleni wakiwa  na njaa kwani huenda wanakosa chakula.

Mwalimu huyo mkuu ameomba wafadhili wengine kujitolea na kuisaidia shule za msingi na misaada mbalimbali ili kuinua viwango vya masomo .

Kwa upande wake mwanasiasa  Mokaya Maroko alikiri  kuwa yeye yuko tayari kushirikiana na wazazi wote  wa shule mbalimbali   katika wadi hiyo ya Gesima ili kuinua viwango vya masomo .

 “Niko tayari kushirikiana na wazazi wote ili kuinua viwango  vya  masoma na  kuwapa wanafunzi motisha ya kufanya  bidii masomoni.