Wakazi wote wa kaunti ya Kisii wameombwa kudumisha na kulinda mila na utamaduni wao kama njia moja ya kukumbuka mambo yanayofanyika.

Share news tips with us here at Hivisasa

Akiwahutubia wanahabari katika jingo moja la utamaduni lililoko Karibu na Shule ya upili ya Kisii, mwenyekiti wa  wazee na utamaduni wa Kisii  Mzee James Matundura aliwaomba wakazi wote kudumisha na kulinda utamaduni wao.

Aidha,aliwaomba viongozi wote wa Kisii kuungana pamoja na kuendeleza miradi mbali mbali ambayo itainua jamiii na kuweka tafouti zao kando ili kufanya maendeleo kwa wananchi waliowachagua.

“Nawaomba viongozi wote kuungana pamoja na kuendeleza miradi mbali mbali katika kaunti yetu hasa sekta ya kitamaduni,” alihoji mzee Matundura

Kulingana na Mzee huyo, Kaunti ya Kisii inastahili kuwa na kivutio cha watalii na vifaa vya utamaduni viwe  huko, ili sekta ya utalii inawiri katika kaunti ya Kisii.

Kwingineko, aalimpongeza Gavana wa kaunti ya Kisii kwa Juhudi anazofanya za  kuinua viwango vya utamaduni, hasa baada ya Ongwae kumkabidhi Rais kifaa cha utamaduni wa Abagusii, wakati wa kongamano la magavana wiki iliyopita.

Matundura amelipongeza  bunge la Kaunti ya  Kisii kwa kupitisha mswada wa kaunti  kuwa na bendera yake ambayo iko na nembo za kitamaduni, kama mdwara amhao unaonyesha umoja wa jamii ya wakisii.

“Napongeza bunge letu la kaunti la Kisii kwa kupitisha mswada wa kuwa na bendera ya kaunti na kuweka nembo za kitamaduni katika bendera hiyo kuashiria kuwa wanapenda kaunti yao,” aliongezea Matundura.