Gavana James Ongwae amewaomba wakazi wote wa kaunti ya Kisii na vikundi mbali mbali kujiandikisha katika kaunti hiyo ili wasimamizi wa kaunti hiyo waweze kuweka mikakati ya kuwaafikia na kutoa  funzo maalumu kwao jinsi ya kujiendeleza kimaisha.

Do you have a lead on a newsworthy story? Share news tips with us here at Hivisasa!

Akiongea jana katika ukumbi wa kitamaduni mjini Kisii, wakati wa kujibu baadhi ya  maswali yalikua yokiulizwa na wakazi walihoudhulia kikao hicho, alisema kuwa kuna  umuhimu wa  kujua baadhi ya vikundi mbali mbali ili  kuwasaidia kutoa  mafunzo maalumu kwao hasa jinsi ya kujua  mipango  ya serikali ya kaunti ya Kisii.

"kuna umuhimu wa Kujulisha na kufahamisha wakazi wote jinsi serikali imeweka mikakati yao kwa wakazi wao na hayo yatawezekana wakati tutatambua vikundi  mbali mbali ili kurahisisha kuwafikia,” alihoji Ongwae 

Ongwae alitaka makundi kama yale ya kinamama,wanabodaboda na sekta ya uchukuzi (matatu) kujiweka pamoja ili waweze kufikiwa na kupewa funzo maalumu jinsi ya kushirikian na kaunti  na kijiimarisha kimaisha.

Aidha, aliwauliza mawaziri wake kuanza kutambua na kuandikisha  makundi hayo kwa  mafunzo hayo.

"Nawaamuliza mawaziri wangu wote wa kaunti  kuanza kutambua na kuandikisha makundi hayo ili tuweze kupata idadi kamili na kupanga  jinsi ya kuwafikia na kuanza kutoa mafunzo hayo," aliongezea Ongwae.

Haya yote ni kutokana na kulalama kwa baadhi ya wakazi wa kaunti ya Kisii, kuwa bado hawajafikiwa na kupata  mafunzo hayo ili kujua ni yapi Serikali hiyo imepanga kuyatekeleza  kwa wakazi wa Kaunti hiyo.

Kwingineko aliwaomba wakazi wote kushirikiana na serikali yake ili kuendelea kufanya kazi kwa pamoja na kuinua viwango vya maendeleo.

kulingana na  Gavana Ongwae hata kama serikali ya kaunti ya Kisii iliorodheshwa kuwa la sita  bora kati ya kaunti ambazo  zimefanya bora alisema kuwa yeye atahakikisha kuwa kaunti ya Kisii inaorodheshwa  ya Kwanza katika utafiti ujao.