Wanakijiji wa Nyamage katika Kaunti ya Kisii walipigwa na butwaa pale ambapo kisa kinachoaminika kuwa cha mazingaombwe ya aina yake kilipotokea mnamo siku ya Alhamisi.

Do you have a lead on a newsworthy story? Share news tips with us here at Hivisasa!

Kulingana na wanakijiji hao, daktari mmoja wa kienyeji alitumia mdomo wake kuwanyonya damu watu walioshukiwa kuwa na uchawi ili kupima kiwango chao.

Daktari  huyo  kwa  jina  Dinah  Moraa  alialikwa  na  naibu  wa chifu wa eneo hilo Sarah Mokua kufuatia visa vingi vya uchawi  wa aina hiyo kukithiri kwa siku za hivi karibuni.

“Mimi kama  naibu  chifu  wenu, kutokana na  visa vingi vya ‘uchawi  wa macho’  vilivyoripotiwa  afisini  mwangu, nilionelea  ni  vyema  nitafute  daktari  ili  atusaidie  kwa  sababu  tatizo  hili  linaumiza  watoto  kwa  watu  wazima  na  hata  husababisha  vifo kama mnavyojua,” alisema Mokua.

Daktari  huyo alisema ya  kwamba kuna  njia  nyingi  za  kupokezwa  uchawi  huo wa macho hata bila muathirika kujua.

“Mchawi  anaweza  kukupokeza uchawi  huo  kwa kukukanyaga  katika  kidole  kikubwa  cha  mguu, kukutwika  au   kumtwika  kitu  kama  maji au  kuni, anaweza  kutia  uchawi  wake  ndani  ya  maji  ya  kupika  yaliyoinjikwa  kwenye  jiko  na  uchawi  huo  utamwingia  kwa  damu pale joto lile la  maji  moto litamuingia  atakayepika  huku  akitokwa  na  jasho,  pia  njia  nyingine ni ya  kubadilishana pesa  za  sarafu,” aliongeza Mokua.

“Pia wachawi  wa  aina  hii wanaweza  kumwagilia  nguo  zilizoanikwa  ama  kumwagilia  mtu  moja kwa  moja  kwa  kumtazama  tu  kwa  macho, yaani kuonana  macho kwa macho,” alihoji Daktari huyo.

Daktari huyo wa kienyeji alitumia nyembe kwa  kumenya vipaji  vya  nyuso  za  watu na kumumunya damu kisha kuitema  kwa kartasi nyeupe. Vidudu  vingetokezea papo hapo na kujigeuzageuza  kwa  kartasi  hiyo  kama  mtu  huyo ana  ule uchawi, na kithibitisha tosha kwamba yeye ni muadhirika, yaani mchawi.

Kati  ya  watu  kadri  ya  arobaini  waliopimwa, sita  walipatikana  na  tatizo  hilo, kasha wakaagizwa  kununua  kondoo mmoja  na  kuku  mwenye  anataga  ama  mwenye  ana  vifaranga  ili  wanyama  hao watumike  kwa  matambiko ya kuwasafisha uchawi huo.

“Sasa mmejionea wenyewe, basi itabidi mnunue  kondoo  na  kuku  anayetaga  ama  awe  ana  vifaranga  ili  wanyama  hao  watumike  kutambika. Damu  yao  na  ngozi  ya  kondoo  huyo  itatumika  kuosha  uchawi  ulio  miilini  mwenu,” aliagiza Daktari.