Wanabodaboda wote katika mji wa Kisii na viunga vyake wameombwa kuwa  na uwazi na wateja wao hasa wakati wakulipwa na wateja wao ili kuepuka mizozo ya pesa na wateja wao.

Share news tips with us here at Hivisasa

Wakiongea katika eneo la Mashauri  kaunti ya Kisii,  baadhi ya wateja walilalama  kuwa wanabodaboda wengi huwa vigeugeu kwa wateja wao wakati wamewafikisha wanakoenda  na kuwadai pesa zaidi ya walizoelewana.

“Nimeghadhabishwa na mwanabodaboda ambaye alinibeba asubuhi ya leo kutoka kituo cha Menyikwa  na kunifikisha hapa kwa sababu alinidai pesa zaidi ya tulizoelewana naye  kutoka  Menyikwa,” alisema James Gichana  mwanafunzi  wa chuo kimoja mjini Kisii.

Aidha amewaomba wanabodaboda hao  kuwa na uwazi wanapopewa pesa hasa  noti na kurudisha salio kulingana na jinsi walivyoelewana na mteja wake.

“Tunajua pikipiki katika usafiri ni haraka kuliko gari kwa kuwa mimi kama mwanabiashara huwa nataka kufika sokoni mapema kwa hivyo ninaomba wanabodaboda na sisi kama wateja kuelewana ili uchukuzi katika mji wetu uendelee vizuri,” alihoji Jospheni Gesare mwanabiashara .

Kwa upande wa wanabodaboda wamewalaumu wateja wao kwa kile walisema kuwa wateja wao huelewana bei na wakati wanawafikisha mahali walielewana, wateja wao ugeuka na hutoa pesa kidogo .

“Tunaelewana  bei na wateja wetu lakini tukiwafikisha mahali wanastahili kufikishwa hugeuka na kutoa pesa kidogo sisi wanaboda boda ndio twawekewa lawama si mteja,’’alielezea  Fred Bosire mwanabodaboda.

Wanabodaboda hao wamewaomba wateja  wao kuwajibika na kazi yao ili kuepuka na mizozo kama hiyo.