Wanabodaboda wote kutoka  kaunti ya Kisii wameombwa kutotumiwa na wanasiasa ili wanasiasa hoa kijinufaisha wenyewe na kuwacha wanabobaboda hivyo bila kujali masilahi yao.

Share news tips with us here at Hivisasa

Akiongea  jana katika hafla ya uzinduzi wa bendera ya kaunti ya Kisii, katika uga wa Gusii, mwenyekiti wa wanabodaboda hao, Mike Mose, aliwaomba vijana hao kuepukana  na wanasiasa walio na nia ya kuwatumia kwa njia ya kujinufahisha wenyewe bila kujjali masaibu na changamoto wanazopitia wakati wanapofanya biashara zao za uchukuzi.

“Nawaomba wanabobaboda wote wa kaunti ya Kisii kutotumiwa na wanasaiasa kwa njia ya kuwapotoza. Jambo hilo linaweza kufanya mpoteze kazi zenu na bidii kwa kazi mnayoifanya,” alisema Mose.

Aidha, aliwataka wanasiasa wajue kuwa vijana hoa huwa  na changamoto  nyingi hasa baridi  wakati wanapofanya biashara na wengi wao wameajiriwa na wamiliki wa  pikipiki ambao huitaji pesa zao kila siku.

Mose alipongeza serikali ya kaunti ya Kisii kwa ushirikiano wao mwema na vijana wa bodaboda huku akisema kuwa yeye na vijana  hao wataendelea kushirikiana na serikali ili kuhakikisha  maendeleo  yamefanywa kupitia sekta ya uchukuzi.

Alitaja sekta ya bodaboda kuwa  bora katika  Kaunti ya Kisii  kwani hata wale wanaofanya kazi kwa ofisi ya serikali ya kaunti hutumia pikipiki ili kufika kazini mapema.

Wanabodaboda wa  Kisii kwa sasa wako na ushirikiano mwema na Serikali hiyo kwa kuwa Serikali hiyo, ikiongozwa na Gavana James Ongwae, iliwasaidia vijana hao kuwa na muungano (Sacco) ambao utawasaidia vijana hao kujiendeleza kimaisha  hasa kupata mikopo.