Mwanamme mwenye umri wa miaka 40, alijitoa uhai Alhamisi kwa kujikata koo katika kitongoji cha Mastoo eneo bunge la Bahati.
Yadaiwa marehemu Peter Ng’ethe aliwahi kujaribu kujitoa uhai mwezi Oktoba 2015, lakini akaokolewa na familia yake na kupelekwa hospitalini.
Ng’ethe na ambaye ni baba ya mtoto mmoja alipatikana na mamake mzazi kama ameaga nyumbani kwake baada ya kuhisi hatari, wakati mlango wa nyumba yake ulipokaa wazi kwa muda mrefu.
Akidhibitisha kisa hicho Chifu wa eneo hilo Mary Muthoni amesema kwamba kisu kikali kilipatikana karibu na mwili wake na michirizi ya damu kutoka shingoni.
“Tunajaribu kutegua kitendawili cha ni kwa nini aijitoa uhai, sababu hakuna fununu kwamba alikuwa amekosana na familia yake. Hata hivyo ni bora kutafuta ushauri kama mtu anasongwa na matatizo, kuliko kujitoa uhai,” aliema Bii Muthoni.
Mwili wake ulichukuliwa na maafia wa polisi wa Githioro na kupelekwa katika ufuo wa hospitali kuu ya Nakuru.