Wizara ya Mazingira na Mali asili inaunda mikakati ya kuhifadhi asilimia kumi ya  misitu katika hatua ya kukabiliana na hali ya anga  kwa kuhusisha jamii zinazoishi kandokando mwa misitu.

Do you have a lead on a newsworthy story? Share news tips with us here at Hivisasa!

Kulingana na katibu katika wizara ya mazingira na mali asili Richard Lesiyampe, serikali inalenga kuhifadhi misitu yake nchini sawia na kuhakikisha kuwa haki za jamii wanaotegemea misitu kwa maisha yao ya kila siku imelindwa.

Akiongea mjini Nakuru, Lesiyampe amesema kuwa  upungufu wa mikakati mwafaka  kwa  jamii zinapelekea  uhaba wa vyakula sawia na kukauka kwa mito nchini

“Hapo awali, wizara ya mazingira ilikumbwa na  changamoto ya kuweka sheria za  kukabiliana na hali ya hewa kutokana na kukosa ufahamu kwa  jamii ya Ogiek na Segwer, kuhusu haki zao kwa rasilimali za misitu kwani  sasa kunaushirikianao kati ya jamii hizo na serikali,” alidokeza Lesiyampe.

Amehoji kuwa migogoro kati ya wananchi na Wanyama pori inaongezeka kila kuchao, kufuatia  mbinu duni za  kuhifadhi mazingira. Hata hivyo, amehoji kuwa  kubadilika kwa minara ya misitu na maji  itaimarisha maendeleo sawia na kupunguza visa vya migogoro miongoni mwa jamii

Hata hivyo, ameonya jamii zinazopigania kuishi kandokando mwa misitu dhidi ya uharibifu, akisema wanapaswa kukuza maendeleo na kujiingiza katika shughuli za kuongeza pato badala ya kusisitiza katika kuishi kandokando mwa misitu.