[Picha/thestar.co.ke]

Share news tips with us here at Hivisasa

Wafanyibiashara katika wanaoendeleza biashara zao katika soko la  Kongowea wametakiwa kutolipa kodi mpaka pale watakapo pata huduma bora katika soko hilo.

 

Akiwahutubia wakaazi wa Mombasa katika majengo ya soko  hilo siku ya jumatatu  hilo Rais Uhuru Kenyatta amesema kuwa hataruhusu kamwe kuona wananchi wananyanyaswa .

 

Uhuru hata hivyo ameongezea kuwa yeyeto atakayepatikana  akiwalipisha kodi wafanyibiashara katika soko hilo watachukuliwa hatua za kisheria.

Kiongozi wa nchi aidha amemtaka mshirikishi wa utawala ukanda wa pwani kukabiliana na  watoza ushuru bandia katika soko hilo la sivyo apigwe kalamu.

Hata hivyo ameahidi kwamba vijana wa mradi kwa vijana, NYS,  watasafisha soko hilo ili kuona kwamba wafanyibiashara wanapata mazingira bora kwenye biashara zao.

Rais aliwapiga marufuku askari wa kaunti ya mombasa kukukusanya ushuru wa soko hilo kwa sababu huduma ni mbovu.