Viongozi wa wa wadi mbalimbali wametakiwa kuzingatia watoto maskini na walio na matokeo ya kufana wakati wa kupeana  hela za kuwasaidia masomoni ili kufanikisha zoezi hilo.

Share news tips with us here at Hivisasa

Haya ni matamshi yake gavana wa jimbo la Nakuru Kinuthia Mbugua katika hafla ya kuwahisani wanafunzi kumi na wawili  kutoka familia maskini katika  jimbo la nakuru ili  kuwawezesha kujinga na shule za upili.

Katika taarifa yake, Gavana huyo amesema kuwa serikali yake itazidi kuwekeza katika sekta ya  Elimu sawia na Afya kama njia moja ya kukabiliana na kero la umaskini katika jimbo.

 Wanafunzi hao aidha waliojumuisha wasichana watatu na wavulana tisa  ni miongoni wa maelfu ambao walipata nafasi za kujiunga na shule za kitaifa  na kukosa uwezo  kwa kuzingatia hali yao ya maisha.

Akiongea katika hafla hiyo,  waziri wa elimu katika jimbo la nakuru Catherine Kitetu amewapa changamoto washikadau sawia na wawekezaji katika jimbo kutoa msaada yao kwa wanafunzi kama hao, akitaja kuwa wengi wa waliofuzu katika mtihani huo ni wale kutokaa familia maskini.

Kitetu aidha amewahimiza wazazi kuhakikisha kuwa wale wanafunzi ambao hawakupata nafasi katika shule za upili kufuatia matokeo yao duni wamejiandikisha ili kupata nafasi katika vyuo vya anuai.

Vilevile, naibu wa gavana Joseph Rutto amewapa changamoto viongozi wengine  katika jimbo na hata serikali kuu  kujitolea na kuwasaidia baadhi ya wanafunzi wanaohitaji msaada  na wala sio  kungojea kukosoa huduma zinazotolewa na wengine .

 Hata hivyo, chini ya mpango ‘Kinuthia Mbugua Foundation’, wanafunzi hao walipokea shilingi elfu mia nane za kuwawezesha masomo yao ya mwaka huu.