Kampuni ya Peak Tracking Limited ni moja kati ya makampuni tano yanayoweka vidhibiti mwendo kwa magari.

Do you have a lead on a newsworthy story? Share news tips with us here at Hivisasa!

Vifaa hivi vinagharimu baina ya shilingi 10,000  na shilingi 30,000 kutegemea na mtoa huduma hiyo.

Mfumo huo wa usalama ni pamoja na teknolojia ya kuonekana kitu kilipo duniani ambacho kinawasaidia watumiaji kugundua wapi vilipo vyombo vyao.

"Teknolojia hii inawaruhusu wamiliki kupelekewa taarifa wakati matukio yasiyotarajiwa kama vile ajali au kuingiliwa nyumbani kunapotokea," mkurugenzi mtendaji wa Peak Tracking Kelvin Macharia anasema.

Akiongea na mwandishi huyu alidokeza: "Ikiwa mwizi anavunja chombo, vifaa vya kuhisi vinatambua tukio hilo na hutuma tahadhari katika simu ya mwenye chombo. Mmiliki anaweza kuita vyombo vya kusimamia sheria, jambo linaloweza kupelekea kutiwa mbaroni, au wanaweza kukifanya chombo kisifanye kazi kwa kutuma ujumbe."

Teknolojia hii pia inawaruhusu wamiliki kuangalia hali ya betri ya gari yao na mfumo wa kiyoyozi wa gari, na hata kusikiza mazungumzo ya watu waliomo katika gari, alisema.

Macharia alisema kuwa zaidi ya wateja 200, wakiwemo watu binafsi na mashirika, wamenunua mfumo huo tangu kampuni yao ilipoanza kutoa huduma hiyo mwezi Januari 2013.

Kampuni ya Peak pia inatoa teknolojia kama hiyo. "Kwa vile teknolojia hii ni mpya kabisa katika soko, wateja wamekuwa wakiongezeka kwa kasi," alisema Morris Mbetsa, ambaye anaongoza kampuni hiyo.

Peak walimwambia mwandishi kuwa kila chombo kinapewa nambari tofauti ili kuhamasisha na kuifanya gari isiweze kufanya kazi ikiwa imeibwa. Watoaji huduma na wanaofunga vifaa hawawezi kupata habari hii.

Ingawaje kumekuwepo na vifaa vingine vya kufuatilia katika soko, alisema teknolojia inayohusiana na simu za mkononi ndiyo pekee ambayo inamruhusu mmiliki wa gari kuwa dhamana mwenyewe.