Zoezi la  kugawa sehemu ambapo zaidi ya wachuuzi 2,000 walioondolewa  kutoka  katikati mwa mji wa Nakuru  na kupelekwa  nyuma ya  barabara  ya Oginga Odinga watakapohudumia inaendelea humo.

Share news tips with us here at Hivisasa

Zoezi hilo linafanywa na viongozi wa kutoka  serikali ya jimbo chini ya ulinzi mkali,  na ambalo limewezesha kwa serikali hiyo kuchukua barabara mbili za umma, ambazo zinadaiwa kunyanukuliwa na watu binafsi.

Aidha, imebainika kuwa  ingawa si wafanyabiashara wote waliofurushwa mjini watapata nafasi katika mahala hapo, serikali ya jimbo la Nakuru imesimama kidete  kwamba wafanyabiashara wote sharti wapate  mahala  mbadala  ambapo watafanyia kazi zao.

Hata hivyo, kwa mjibu wa mmoja wa wachuuzi hao Kahiga Karanja ameikumbatia hatua hiyo akihoji kuwa ni hatua itakayopunguza msongamano mjini huku, akihoji kuwa japo zoezi hilo litalemaza biashara zao kwa muda zitaimarika baadaye

Zoezi hilo linajiri huku upande mmoja wa wachuuzi ukiishtaki serikali ya jimbo na kesi  hiyo ikitarajiwa kusikizwa jumatatu ijayo.